Kongamano lilikuwa kwa ajili ya kuadhimisha jubilei ya watoto katika mwaka Mtakatifu wa Jubilei Kuu 2025. Watoto washiriki walikuwa 2500. Walezi 11, masista 12, mapadre 9, mashemasi 3 na waseminari wawili wa mwaka wa uchungaji Mada zilizofundishwa: 1. Jubilei Kuu 2025, 2. Liturjia Katoliki,3. Lishe. 4. Ulinzi na usalama wa mtoto Majina ya watoa mada: Fr. Erasmo Mligo, Fr, Gabriel Haule, Bi. Bertha Bartholomeo Nyigu, Bi. Alodia Mkinga

Aidha, Kwenda kwenye eneo  la  kongamano  kila  parokia  walitakiwa  kuwafikisha watoto Sekondari ya Josefine. Kwa kulingana na Jografia ya jimbo letu, Parokia za mwambao wa ziwa walianza safari kwa  boti mpaka  kufika  nchi kavu na hatimaye kwa mabasi mpaka eneo la kongamano. Parokia nyingine walikodi mabasi yaliyowaleta mpaka eneo la kongamano. Siku ya kilele, ilitia fora sana. Watoto, masista wachache na walezi waliandamana wakisindikizwa na polisi wa usalama barabarani mpaka jimboni. Baada ya misa walirejea eneo la kongamano  kwa  sherehe za kufunga na hatimaye kurudi Parokiani.

Ni ukweli usiopingika kuwa Watoto walifurahi sana kukutana kama watoto wa jimbo moja na kufanya mambo mbalimbali pamoja. Misa ya ufunguzi wa kongamano iliongozwa na Mkurugenzi wa utume wa Walei Jimbo la Njombe Mhesh Padre Francisco Betes Chengula. Misa ya kufunga kongamano iliongozwa na Mhashamu Eusebio Samwel Kyando. 10. Watoto waliagizwa kusoma lnjili yote ya Yohane na kutoka humo walikuwa na mashindano ya kujibu maswali. Aidha, kulikuwa na mashindano ya lgizo lililotoka katika lnjili hiyohiyo na shindano la Kwaya.Wimbo ulioshindaniwa umefanywa kuwa Wimbo wa Utoto Mtakatifu Jimbo Katoliki la Njombe kwani watoto wote jimbo zima wanaweza kuuimba. Baada ya mashindano tuliutangaza rasmi kuwa ndio wimbo wa Utoto Mt Jimbo. Tuliagiza kila Parokia watoto wakutananpo kwa sala au michezo uimbwe kwanza. Kulikuwa pia na ngoma za asili za burudani toka Ukisi,Mwambao wa Ziwa Nyasa, Upangwa na Ubena.

Kongamano letu halikuwa la kikanda . llikuwa ni jubi lei ya watoto wa jimbo la Njombe katika mwaka Mtakatifu ambapo makundi mbalimbali ya kikanisa wanaaadhimisha mfano mapadre, watawa, wana ndoa, vijana ,wasemi nari nk. Sasa kwa upande wa watoto imefanyika ushiriki na ufanisi mkubwa zaidi- ya kundi lolote. Parokia zote SO za jimbo zilikuwa na wawakilishi. Ohamira ya kongamano ikiwa ‘mletee mtoto katika njia ipasayo, naye hataiacha hata atakapokuwa mzee’ Mith 22:6. Mimi kama mlezi nilifurahiswa zaidi na mambo matatu; kwanza ushiriki mkubwa wa watoto. Pili, watoto walivyofurahi hasa siku ya kilele licha ya baridi kali ya Njombe na tatu, jinsi watoto walivyochangamkia mada walizokuwa wanafundishwa hasa mada iliyohusu ulinzi na usalama wao.

Tunamshukuru sana Mungu kwa kutuwezesha kufanya kazi hii iliyotukuka ya kimisionari; bila kupata changamoto ya pekee. Pili, tunamshukuru sana Mhashamu Baba Askofu Kyando kwa kuruhusu niitishe kongamano hili iii kuweka alama katika mwaka huu wa Jubilei Kuu 2025 . Nawashukuru mapadlre, watawa, makatekista,walezi wa watoto na waza zi kwa maandaliz i yote waliyofanya hata kunifanya nionekane nimefaulu; kwa kweli wao ndio waliofaulu. Mimi nilikuwa mratibu tu. Mwisho, lakini si kwa umuhimu nawashukuru Ofisi ya PMS Taifa kwa kutuhamasisha kufanya shughuli hizi iii kung’arisha umisionari wa watoto. Hamasa yenu ndiyo iliyonisukuwa kujasiria mambo haya matakatifu.

 

 

 

Imetayarishwa na: Pd. Julius Mgaya, Mkurugenzi PMS Jimbo