Watoto wa 402 wa Parokia ya Lundumato walifanya kongamano la kiparokia, kuanzia tarehe 20-24 Agosti, 2025. Kwa muda wote wa Kongamano watoto walikuwa kupata semina mbalimbali za kuwajenga kiroho na kimaadili. Tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwamba tarehe 23 siku ya Jumamosi, watoto waliweza kujiunga na kanisa la Tanzania kwa lengo la kuombea Haki na Amani vitawale, hasa katika uchaguzi mkuu wa viongozi unaotarajiwa kufanyika mwaka huu. Kwahiyo, Pamoja na nia hiyo muhimu, walifundishwa mada 2 ambazo ni, Historia ya Shirika la Kipapa na Muundo wake na Maisha ya Wito na Sala.
Kwa kutambua kuwa walezi ni nguzo katika kusimama na kukua kwa shirika hili, walifundishwa mada ya Ulinzi wa mtoto ili wapate ujuzi wa kuwalinda watoto katika utume wao wa kulea. Idadi ya watoto walioshiriki kongamano ni 402.
Jumamosi usiku tulikuwa na Saa Takatifu tukiabudu Ekaristi kuamkia Dominika ambayo kongamano lilihitimishwa kwa Misa Takatifu kuombea Haki na Amani.
Imetayarishwa na Pd. Erasto Nyimbo, Mkurugenzi PMS Jimbo
