Mnamo tarehe 19 Juni 2025, zaidi ya watoto 100 kutoka jimbo la Morogoro walifanikiwa kuanza safari yao ya kuelekea Dar es Salaam kwa ajili ya Kushiriki Kongamano la kanda ya mashariki la utoto Mtakatifu ambalo lilikuwa na jumla ya watoto 2567. Aidha, kongamano hili lilijumuishwa na majimbo saba ambayo ni: Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Bagamoyo, Zanzibar, Morogoro, Ifakara, Mahenge, na Tanga.

Kongamano hili lilifanyika katika parokia ya Kristo Mfalme Tabata DSM. Watoto walisafiri kwa njia ya Gari Moshi (Treni). Safari hii kwa watoto ilikuwa ya furaha sana kwani takribani watoto washiriki wote, hii ilikuwa mara yao ya kwanza kusafiri na chombo hiki cha kisasa hapa nchini. Kongamano lilikuwa zuri kwa watoto kwani waliweza kujifunza mambo mengi kwa kipindi chote cha siku tano yaani tarehe 109 23 Juni 2025.

Aliyeadhimisha misa ya ufunguzi alikuwa ni Askofu msaidizi wa jimbo kuu la Dar es Salaam, Henry Mchamungu, akiongozana na mapadre wakurugeni kutoka kanda ya DSM; Pd. Joachim Masangu (Morogoro), Pd. Denis Wigira (Dar es Salaam), Pd. Aidan Kadudu (Bagamoyo), Pd. Haki (Zanzibar), Pd. Julius Mgaichuma (Mahenge), Pd. Michael Mhina (Ifakara), Pd. Paul Semng’indo (Tanga)

Sukrani kwa Mungu kwa kutusafirisha salama. mwenyezi Mungu na awasaidie watoto wetu waendelee kukua katika kumjua Mungu na pia kuwa na ari zaidi ya kuyatimiza matakwa yake.

 

 

 

Imetayarishwa na Pd. Joachim Masangu, Mkurugenzi PMS