Mnamo tarehe 20 Julai, 2025, watoto wa Utoto Mtakatifu pamoja na walezi wao kutoka parokia mbalimbali za jimbo, waliadhimisha misa takatifu kwa ajili ya shukrani kwa Mungu kwa ajili ya Kongamano la kanda ya Mashariki lililofanyika katika Jimbo Kuu la Dar es Salaam tarehe 19 – 23 Juni, 2025. Maadhimisho haya yalifanyika katika parokia ya Maria Consolatha – Sua.

Sambamba na tukio hili la shukrani kwa ajili ya kongamano lililoisha, siku hii pia ilikuwa ni siku rasmi kwa ajili ya kumpongeza na kumkaribisha Padre Joachim Masangu kama mkurugenzi mpya katika Ofisi ya Mashirika ya Kipapa hapa jimboni Morogoro

Aidha, shukrani hizi ziliambatana na tukio la kumuaga Pd. Aidan Kadudu ambaye alikuwa ni mkurugenzi wa mashirika sha Kipapa Jimboni humu. Watoto katika hafla hii waliweza kucheza michezo mbalimbali kwa ajili ya kumuaga pamoja na kumpatia zawadi malimbali.

Padre Kadudu kwa sasa amehamishwa kutoka jimbo la Morogoro kuelekea jimbo la Bagamoyo. PMS Morogoro wanayofuraha kwamba padre Kadudu anaendeleza huko Bagamoyo utume wake ambao alikuwa anaufanya akiwa jimbo la Morogoro wa kusimamia na kuliendeleza shirika la utoto mtakatifu jimboni humo.

 

 

 

 

Imeandaliwa na: Pd. Joachim Masangu, Mkurugenzi PMS Jimbo