Leo tarehe 8 Aprili, 2025 Utoto mtakatifu Jimbo Kuu la Dar es Salaam waliadhimisha misa ya shukrani baada ya kumaliza Kongamano la Kanda ya Mashariki ambalo mwaka huu lilifanyika jimboni DSM kuanzia tarehe 19 –23 Juni, 2025 katika Parokia ya Kristo Mfalme Tabata. Katika kongamano hilo la kikanda, washiriki watoto kutoka majimbo saba (Jimbo kuu la DSM, Jimbo la Bagamoyo, Zanzibar, Tanga, Morogoro, Ifakara na Mahenge), walikuwa takribani 2600.

Misa ya shukrani kwa ajili ya kufanikisha zoezi hilo muhimu ilifanyika katika parokia ya Mt. Peter Clavery – Mbezi Louis. Mwazimishaji wa ibada ya misa takatifu alikuwa ni Padre Denis Agness Wigira, Mkurugenzi wa Mashirika ya Kipapa Jimbo Kuu la Dar es Salaam. Katika homilia yake Pd. Wigira aliwapongeza watoto pamoja na walezi kwa kuchukulia siku hii muhimu kwao kwani shukrani ni jambo muhimu sana katika maisha ya mwanadamu. Hivyo aliwaasa waendelee kuona fahari katika hilo pamoja na kufurahia utume wao wa kimisionari siku zote. Misa hii ilihudhuriwa pia na wawakilishi kutoka Ofisi ya Mashirika ya Kipapa (Sr Anagladness Mrumah, Katibu wa Utoto Mtakatifu Taifa pamoja na Sr Idda John Mketi ambaye ni katibu Muhtasi wa ofisi ya Mashirika ya Kipapa) ili kushirikiana na wanajimbo katika kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa makuu yake aliyowatendea.

 

 

 

Imeandaliwa na Sr Anagladness Mrumah, Katibu wa Utoto Mtakatifu Taifa