Archives for Njombe Diocese

TAARIFA YA KONGAMANO LA UTOTO MTAKATIFU JIMBO LA NJOMBE, 24-28 JUNI, 2025

Kongamano lilikuwa kwa ajili ya kuadhimisha jubilei ya watoto katika mwaka Mtakatifu wa Jubilei Kuu 2025. Watoto washiriki walikuwa 2500. Walezi 11, masista 12, mapadre 9, mashemasi 3 na waseminari wawili wa mwaka wa uchungaji Mada zilizofundishwa: 1. Jubilei Kuu 2025, 2. Liturjia Katoliki,3. Lishe. 4. Ulinzi na usalama wa mtoto Majina ya watoa mada: Fr. Erasmo Mligo, Fr, Gabriel Haule, Bi. Bertha Bartholomeo Nyigu, Bi. Alodia Mkinga

Aidha, Kwenda kwenye eneo  la  kongamano  kila  parokia  walitakiwa  kuwafikisha watoto Sekondari ya Josefine. Kwa kulingana na Jografia ya jimbo letu, Parokia za mwambao wa ziwa walianza safari kwa  boti mpaka  kufika  nchi kavu na hatimaye kwa mabasi mpaka eneo la kongamano. Parokia nyingine walikodi mabasi yaliyowaleta mpaka eneo la kongamano. Siku ya kilele, ilitia fora sana. Watoto, masista wachache na walezi waliandamana wakisindikizwa na polisi wa usalama barabarani mpaka jimboni. Baada ya misa walirejea eneo la kongamano  kwa  sherehe za kufunga na hatimaye kurudi Parokiani.

Ni ukweli usiopingika kuwa Watoto walifurahi sana kukutana kama watoto wa jimbo moja na kufanya mambo mbalimbali pamoja. Misa ya ufunguzi wa kongamano iliongozwa na Mkurugenzi wa utume wa Walei Jimbo la Njombe Mhesh Padre Francisco Betes Chengula. Misa ya kufunga kongamano iliongozwa na Mhashamu Eusebio Samwel Kyando. 10. Watoto waliagizwa kusoma lnjili yote ya Yohane na kutoka humo walikuwa na mashindano ya kujibu maswali. Aidha, kulikuwa na mashindano ya lgizo lililotoka katika lnjili hiyohiyo na shindano la Kwaya.Wimbo ulioshindaniwa umefanywa kuwa Wimbo wa Utoto Mtakatifu Jimbo Katoliki la Njombe kwani watoto wote jimbo zima wanaweza kuuimba. Baada ya mashindano tuliutangaza rasmi kuwa ndio wimbo wa Utoto Mt Jimbo. Tuliagiza kila Parokia watoto wakutananpo kwa sala au michezo uimbwe kwanza. Kulikuwa pia na ngoma za asili za burudani toka Ukisi,Mwambao wa Ziwa Nyasa, Upangwa na Ubena.

Kongamano letu halikuwa la kikanda . llikuwa ni jubi lei ya watoto wa jimbo la Njombe katika mwaka Mtakatifu ambapo makundi mbalimbali ya kikanisa wanaaadhimisha mfano mapadre, watawa, wana ndoa, vijana ,wasemi nari nk. Sasa kwa upande wa watoto imefanyika ushiriki na ufanisi mkubwa zaidi- ya kundi lolote. Parokia zote SO za jimbo zilikuwa na wawakilishi. Ohamira ya kongamano ikiwa ‘mletee mtoto katika njia ipasayo, naye hataiacha hata atakapokuwa mzee’ Mith 22:6. Mimi kama mlezi nilifurahiswa zaidi na mambo matatu; kwanza ushiriki mkubwa wa watoto. Pili, watoto walivyofurahi hasa siku ya kilele licha ya baridi kali ya Njombe na tatu, jinsi watoto walivyochangamkia mada walizokuwa wanafundishwa hasa mada iliyohusu ulinzi na usalama wao.

Tunamshukuru sana Mungu kwa kutuwezesha kufanya kazi hii iliyotukuka ya kimisionari; bila kupata changamoto ya pekee. Pili, tunamshukuru sana Mhashamu Baba Askofu Kyando kwa kuruhusu niitishe kongamano hili iii kuweka alama katika mwaka huu wa Jubilei Kuu 2025 . Nawashukuru mapadlre, watawa, makatekista,walezi wa watoto na waza zi kwa maandaliz i yote waliyofanya hata kunifanya nionekane nimefaulu; kwa kweli wao ndio waliofaulu. Mimi nilikuwa mratibu tu. Mwisho, lakini si kwa umuhimu nawashukuru Ofisi ya PMS Taifa kwa kutuhamasisha kufanya shughuli hizi iii kung’arisha umisionari wa watoto. Hamasa yenu ndiyo iliyonisukuwa kujasiria mambo haya matakatifu.

 

 

 

Imetayarishwa na: Pd. Julius Mgaya, Mkurugenzi PMS Jimbo

 

 

 

 

 

 

Read more

WATOTO WA KIPAPA NA JUBILEI KUU 2025

Katika mwaka huu wa Jubilei kuu, watoto wa JNNK ya Mt. Benedicto, kigango cha Lupingu, Paroki ya Lupingu, Jimbo la Njombe wamefanikiwa kuiweka na kuitekeleza mikakati yao ya kusali Jumuiya Ndogongogo ya Kikristo kwa muda wa wiki sita kwa malengo kadhaa. Watoto hawa kwa muda wa wiki sita wamekuwa katika Umisionari wa kupita katika kila Jumuiya ndogondogo ili kuwahamasisha wenzao kuhusu Mwaka mtakatifu pamoja na kusali sala ya jubilee hii. Pamoja na kusali sala hii, wamekuwa wakifanya tathimini juu ya kazi zao za umisionari ili kuweza kuboresha zaidi utume wao na kuhakikisha kuwa wanapofika katika jumuiya nyingine za watoto wanakuwa wameshaandaa mambo muhimu ya kuwashirikisha.

Aidha, pamoja na sala ya jubilee wanayokuwa wakiisali kila wanapokutana, daima wamekuwa na utamaduni wa kusali sala ya rozari takatifu ili kumuomba mama Maria aliye nyota ya Uinjilishaji, aweze kusafiri nao kwenye utume wao.

 

Imeandaliwa na: Pd. Lucas Mgaya, Mkurugenzi wa PMS – Jimbo

Read more

KONGAMANO LA UTOTO MTAKATIFU JIMBO KATOLIKI LA NJOMBE – 2024

Kuanzia tarehe 26 Desemba 2024, Parokia mbalimbali za jimbo la Njombe; wamefanya makongamano ya Utoto Mtakatifu. Katika Parokia  ya Familia Takatifu-Utalingolo watoto walifundishwa mada zifuatazo: Haki na wajibu wa mtoto-iliyotolewa na Arodia Mkinga, Mtoto mmisionari-ilitolewa na Sr. Lucia Mpete OSB, Liturjia – Pd. Lucas Mgaya

Kulikuwa na mada zilizotolewa kwa walezi: Namna ya kuwafundisha watoto– Sr. Lucia Mpete OSB, Ulinzi na usalama wa mtoto-Arodia Mkinga

Dhamira kuu ya kongamano ilikuwa: Sisi Sote ni Wamisionari.

Jumla ya watoto washiriki katika Parokia mbalimbali ni 1,794 kadiri ya ripoti zilizotumwa katika Ofisi yetu ya PMS Jimbo. Katika kongamano hili, watoto walipata fursa ya kutembelea watoto walemavu na maskini na kuwapelekea zawadi ndogondogo.

 

 

Imeandaliwa na: Pd. Lukas Mgaya, Mkurugenzi wa Mashirika ya Kipapa-Jimbo

 

Read more

TANZANIA – MILLION CHILDREN PRAY THE ROSARY (19 OCTOBER, 2024)

Today the studios of Radio Maria Tanzania roared with the voices of praying the Universal Holy Rosary, while they invited people from every group: elders, youth, businessmen, farmers, and other groups, with the concept of living the message of Pope Francis for Mission Sunday 2024 which says; Go and invite everyone to the banquet (Mt 22:9).

In honor of the Virgin Mary, Star of Evangelization, today October 19, 2024, the children of Tanzania raised their voices together through Radio Maria and other radio stations of the Catholic Church joining spiritually with all the children in the world to pray the holy rosary that is prayed every year in October on the Saturday before Mission Sunday. The specific goal of today’s rosary for the children of Tanzania was to pray for peace, unity and the success of the missionary works in the Local Church of Tanzania and the world at large.

Since it has become a formula for the PMS National Office to choose every year 7 dioceses that take turns in leading others in the rosary, this year the leading dioceses were: Dioceses of Musoma (first mystery), Mahenge (second mystery), Archdiocese of Tabora (third mystery), diocese of Lindi (forth mystery), Mafinga (fifth mystery), Moshi (the litany) and the Archdiocese of Dar es Salaam which is given a chance every year considering that they are close to radio headquarters and if unexpected communication errors occur in a certain diocese they can support (their leading part was the opening and closing prayers).

By comparing the statistics that the PMS National Office has been taking every year to know the number of children who were praying the rosary on the scheduled day and time, the office admits that this year the number of children has been more surprising than previous years. For instance; archdiocese of Arusha gathered about 4000 children, Bukoba 2500, Bunda 500, Dar es Salaam 5000, Dodoma 3000 children, Ifakara 210, Kayanga 230, Moshi 5000 children, Mbulu 6400, Mbeya 6000, 1500 Kahama, Singida 3200 children, Mahenge 500, Njombe 1500, Songea 1900, Lindi 300 children, Iringa 3200, Mafinga 200, Musoma 300 to name a few. There were also priests (Diocesan PMS Directors), nuns and animators who were leading the children in the event of praying the rosary for each diocese. The PMS national team (Fr Alfred S. Kwene – PMS National Director, Sr Idda J. Mketi – PMS Secretary and Sr Anagladness Mrumah – National Childhood Secretary) joined to pray at the main center, that is, Blessed Virgin Mary of Fatima Parish-Msimbazi, where the children of the Archdiocese of Dar es Salaam gathered. Hence, with this assessment that the office has done, it has clearly shown that missionary work in Tanzania is growing and spreading rapidly like the seeds of the sower that fell on good soil (Ref. Mk 4:3-9)

It was a joy for us in Tanzania that we were able to have two bishops joining the children’s rosary (His Eminence Protase Cardinal Rugambwa and Rt. Rev. Jovitus Mwijage). Correspondingly, before the blessing His Eminence Cardinal Rugambwa was able to talk to the children and encourage them in living their missionary work tirelessly. In a special way, he was able to encourage all believers to live the message of the holy father of Mission Sunday 2024, which encourages all people to go and invite everyone wherever they are, so that they can follow Christ.

 

From PMS National Office

 

Read more