Archives for News & Events

THE FEAST OF THE PRESENTATION OF THE LORD IN TANZANIA (1 FEBRUARY, 2025)

Today the Church of Tanzania joined the world church in celebrating the feast of the Presentation of the Lord in the Temple. On this day, hundreds of religious women and men were able to gather together in their dioceses and celebrate the Holy Mass, a celebration in which the nuns had the opportunity to renew their covenants with God, as they had promised earlier.

In fact, this feast has been a deeply reflective one as the celebrants of the mass, who were bishops, were able to touch on matters that are very fundamental in the life of the nuns. For example, in the archdiocese of Dar es Salaam, Auxiliary Bishop Henry Mchamungu, reminded the nuns of several things that the nuns should consider. Among these things he emphasized are: a nun to ensure that he/she becomes a person of prayer and contemplation, living a community life, living a life of penance, living the charisms of the congregation, living a life of dedication, following the rules and regulations of the place where they are given to do a mission and doing a mission for the benefit of the church.

Since in the archdiocese of Dar es Salaam they have the custom of congratulating nuns who in the relevant year are celebrating their jubilees of religious life, on this day, 12 religious women were congratulated; two golden jubilees (Sr Edmunda & Sr Theonestina) and 10 Silver jubilees (Srs Jadwiga, Anagladness Mrumah, Idda John, Elionora Danghalo, Mariel Kazibure, Florence Pontian, Alistidia Faustine, Veronika Mikoma & Ritha Mary).

The Church in Tanzania is proud to have many religious men and women who, with their various charisms, have been able to carry out different missions in the church and thus be able to manifest Christ to his people. Furthermore, we pray that the Lord of the harvest will continue to bring workers into his field.

 

 

Prepared by: PMS National Office

 

 

Read more

SEMINAR WITH ANIMATORS OF THE MAFINGA DIOCESE, JANUARY 3, 2025

The National PMS Office thank God for having the opportunity to participate in the Diocesan Holy Childhood Congress which started on January 31-01, 2025. As is the case with other diocesans, on behalf of the National PMS Office, Sr Anagladness Mrumah who is the secretary of Holy Childhood at the national level, admits to be very happy with this first Congress of Holy Childhood diocesan level, which has been successful with high efficiency.

In addition, in this Congress, the office had the opportunity to give a seminar to two groups, namely: a group of children whose number was 902 and a group of children’s animators who were 74. The topic given to children was about Pontifical Mission Societies and in a very special way on of the Pontifical Mission Societies of the Holy Childhood. The topic for animators was about the important things that they should follow in their parenting work.

Therefore, in a general assessment, this first congress which has been held under the leadership of Fr Gosbert Mlambia, has built a very solid foundation for future congresses in this diocese and thus make missionary work grow rapidly in this diocese.

 

 

Prepared by: National PMS Office

Read more

JIMBO KUU LA MBEYA KONGAMANO LA UTOTO MTAKATIFU 27-30 DEC. 2024

Kongamano la utoto Mtakatifu lilifanyika Katika Parokia ya Mt. Francisco wa Assis Mwanjelwa huku tukitumia majengo ya Chuo Kikuu (CUoM) Kwa malazi na vipindi kwa watoto wetu. Kaulimbiu ya Kongamano letu ni “ULINZI WA MTOTO NI JUKUMU LANGU NA LAKO

Idadi ya washiriki ilikuwa kama ifuatavyo; Watoto wa Kipapa 2908, Mapadre 5, Watawa 15, Walezi 241 na Askofu 1

 

Tulianza Kongamano kwa Misa Takatifu iliyoongozwa na Mhasham Askofu Msaidizi Godfrey mwasekaga mnamo tarehe 28.12.2024 asubuhi kisha ikafuata rariba ya vipindi mbalimbali. Mada zilizofundishwa ni pamoja na;

  1. Ulinzi wa Mtoto (Mapadre, Watawa, RPC na wadau waalikwa)
  2. Mtoto na sala (Mapadre na Watawa walioandaliwa)
  3. Ekaristi Takatifu chemichemi ya Maadili mema kwa watoto. (Mapadre)

 

Sambamba na mada hizo zilizotolewa, kulikuwa na burudani mbalimbali kwa watoto kama vile ngoma, vichekesho, maigizo, muziki, ngonjela na nyimbo.

Zawadi mbalimbali zilitolewa kwa waliofanya vizuri ili kuamsha ari ya kujiandaa vizuri wakati wa Kongamano.

 

Kwa upande wa Liturjia, watoto walihudumu vizuri na kwa zamu. Walishiriki vema katika Uimbaji wakati wa Misa, wengine walihudumu altareni na wengine walitumikia kwa nafasi mbalimbali wakati wa Misa. Siku ya kilele kulikuwa na maandamano yaliyoongozwa na Mhasham Askofu Msaidizi Godfrey Mwasekaga kuanzia Kanisa la kiaskofu Jimboni hadi Mwanjelwa. Tuliandamana vizuri bila kupata changamoto yeyote na kisha tukahitimisha kwa Misa Takatifu. Kwa ujumla vitu vyote vilifanyika vizuri bila kupata changamoto kubwa kwa watoto wetu.

Tunashukuru kwa miongozo mbali mbali tunayoipata kutoka Ofisi ya Taifa. Mungu awabariki.

 

 

Imeandaliwa na: Fr. Exavery Maingu Mafwimbo

Mkurugenzi PMS Jimbo Kuu la Mbeya

Read more

SEMINAR WITH ANIMATORS OF THE MAFINGA DIOCESE, JANUARY 3, 2025

 

 

In a special way, the National PMS Office thank God for having the opportunity to participate in the Diocesan Holy Childhood Congress which started on January 31-01, 2025. As is the case with other diocesans, on behalf of the National PMS Office, Sr Anagladness Mrumah who is the secretary of Holy Childhood at the national level, admits to be very happy with this first Congress of Holy Childhood diocesan level, which has been successful with high efficiency.

In addition, in this Congress, the office had the opportunity to give a seminar to two groups, namely: a group of children whose number was 902 and a group of children’s animators who were 74. The topic given to children was about Pontifical Mission Societies and in a very special way on of the Pontifical Mission Societies of the Holy Childhood. The topic for animators was about the important things that they should follow in their parenting work.

Therefore, in a general assessment, this first congress which has been held under the leadership of Fr Gosbert Mlambia, has built a very solid foundation for future congresses in this diocese and thus make missionary work grow rapidly in this diocese.

 

 

 

 

Prepared by: PMS National Office

Read more

KONGAMANO LA UTOTO MTAKATIFU JIMBONI IFAKARA, 2024

Mwaka huu kongamano la utoto mtakatifu katika jimbo la Ifakara, limefanyika katika parokia ya mtakatifu Francis Xavery Kisawasawa kuanzia tarehe 26-28 Disemba 2024. Kongamano hili lilikuwa na jumla ya washiriki watoto wapatao 591. Kauli mbiu ya kongamano hili ilikuwa ni Mtoto ni Malezi. Aidha, mada mbalimbali ziliwasilishwa na watu wafuatao: Uelewa juu ya Biblia Takatifu na Maadili Mema na Pd. Boniface Mwanja, Sakramenti za Kanisa na Ekaristi takatifu Pd. Edson Lyabonga.

Kongamano hili pia lilinogeshwa na maandamano ya kimisionari ambayo yalifanyika siku ya tarehe 28 na kupokelewa na baba Askofu Salitarus Libena, na baadaye misa takatifu ya Watoto Mashahidi.

Tunamshukuru sdana Mungu aliyeyawezesha haya yakaweza kufanyika kwa kadiri ya mpango wake.

 

 

 

 

 

Imeandaliwa na: Pd. Michael Mhina, Mkurugenzi wa Mashirika ya Kipapa, Jimbo

Read more

KONGAMANO LA UTOTO MTAKATIFU JIMBONI LINDI (26-28 DEC. 2024)

Watoto wa jimbo katoliki la Lindi wameweza kushiriki kongamano lao hapo Disemba  mwaka huu 2024, katika parokia ya Kilwa Masoko. Kongamano hili lilianza mnamo tarehe 26 – 28 Disemba (sikukuu ya watoto mashahidi). Washiriki watoto katika kongamano hili walikuwa jumla yao 410 kutoka katika kila parokia.

Katika kongamano hili watoto walifundishwa mada mbalimbali kama ifuatavyo: Jografia ya Biblia na Pd. Paul Chembe, Mkurugenzi wa Mashirika ya Kipapa Jimbo, Haki na wajibu wa mtoto na Pd. Fridolin Makwinya, Liturujia Ibada ya Misa Takatifu na Sr. Tereza Awino na mada juu ya Malezi ya Watoto iliwasilishwa na Mariam Mlacha.

Aidha katika kilele cha kongamano hilo, kulikuwa na maandamano ya watoto yaliyokuwa na lengo la kusambaza mbegu ya uinjilishaji, kwanza kwa watoto wengine ambao bado hawajamfahamu Mungu bado lakini pia kwa watu wote. Ni katika maamdamano haya, kwa bahati nzuri baba Askofu Wolfgang Pisa OFM Cap wa jimbo la Lindi na Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, aliweza kufanya maandamano pamoja na watoto na kwa namna ya pekee kuongoza misa katika kilele cha kongamano hilo.  Hakika, katika kongamano hili ni dhahiri kabisa kuwa watoto walisia mbegu ya uinjilishaji, kwao binafsi na kwa wengine waliokuwa nje ya kundi hili.

 

 

 

Imeandaliwa na: Pd. Paul Chembe, Mkurugenzi wa Mashirika ya Kipapa-Jimbo

Read more

KONGAMANO LA UTOTO MTAKATIFU JIMBONI SAME TAREHE 10-13/12/2024

Tunamshukuru Mungu kwa zawadi ya uhai na baraka nyingi alizotujalia mwaka huu.Tunamshukuru pia kufanikisha uwepo wetu katika kongamano letu la Utoto Mtakatifu. Tunamshukuru mlezi wetu mkuu yaani Baba Askofu kwa kutupa nafasi ya kukua katika malezi kwani “mtoto ni malezi” Mwaka huu tulifanikiwa kuleta nyumbani wazo la Kongamano la tano la Ekarestia kitaifa kwa kuwakutanisha Watoto wapatao 933 na walezi 76 jumla 1009 kwenye viwanja vya uaskofuni kwa muda wa siku nne.

Aidha, mada zilizowasilishwa kwa watoto ni pamoja na: Undugu huponya ulimwengu (Na Mwl. Silvano), Imani Katoliki (Na Mwl. Festo Hiza), Mtoto Mmisionari na uwajibikaji – Elimu, Wajibu na matokeo yake (Na Mwl. Silvano)Namna ya kuishi maisha ya furaha ukiwa Mtoto (Na Mwl. Festo Hiza), Haki ya Mtoto mmisionari kwa Kanisa na Taifa (Na Mwl. Silvano) Maisha ya Mtoto mmisionari kwa Watoto wenzake (Na Mwl. Festo Hiza),  Mashindano ya usomaji wa Biblia (Na Mwl. Silvano na Walezi Msista)

 

Walezi wa Utoto Mtakatifu walifundishwa ama kukumbushiwa juu ya Wajibu wa Mlezi katika Malezi (Na Mwl. Silvano)

MAFANIKIO

Watoto wamepata Malezi na mafundisho mblimbali kulingana na dhamira ya kongamano hususani Undugu unaoponya Ulimwengu na athari za kutokutambua haki za Mtoto. Walipata pia Sakramenti kama vile sakramenti ya Kitubio na Ekaresti Takatifu

MAPENDEKEZO YA WATOTO

  1. Watoto walipendekeza kuwa Walezi wawe na Kongamano lao wenyewe kutangulia kongamano la Watoto. Hii itawafanya kutoa malezi vizuri ikiwa wanajua wanachokifanya.
  2. Watoto walipendekeza kuwa Wazazi wasiwazuie Watoto wenzao kuja kongamano
  3. Watoto waliomba kuvumiliwa kwa usumbufu wao na changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika malezi.

MWISHO

Siku ya kilele tulifanya Maandamano kabla ya adhimisho la Misa Takatifu ikiwa ni fursa kwa Watoto kuinjilisha kwa vitendo. Hakika tumeonja Uwepo wa Utukufu na Upendo wa Mungu kati ya Watoto na Walezi waliponywa na Yesu wa Ekaresti. Yote kwa Utukufu Wake.

 

Imeandaliwa na: Pd. Alphonce Ndaghine, Mkurugenzi wa Mashirika ya Kipapa – Jimbo  

                                            

Read more

KONGAMANO LA UTOTO MTAKATIFU JIMBO KATOLIKI LA NJOMBE – 2024

Kuanzia tarehe 26 Desemba 2024, Parokia mbalimbali za jimbo la Njombe; wamefanya makongamano ya Utoto Mtakatifu. Katika Parokia  ya Familia Takatifu-Utalingolo watoto walifundishwa mada zifuatazo: Haki na wajibu wa mtoto-iliyotolewa na Arodia Mkinga, Mtoto mmisionari-ilitolewa na Sr. Lucia Mpete OSB, Liturjia – Pd. Lucas Mgaya

Kulikuwa na mada zilizotolewa kwa walezi: Namna ya kuwafundisha watoto– Sr. Lucia Mpete OSB, Ulinzi na usalama wa mtoto-Arodia Mkinga

Dhamira kuu ya kongamano ilikuwa: Sisi Sote ni Wamisionari.

Jumla ya watoto washiriki katika Parokia mbalimbali ni 1,794 kadiri ya ripoti zilizotumwa katika Ofisi yetu ya PMS Jimbo. Katika kongamano hili, watoto walipata fursa ya kutembelea watoto walemavu na maskini na kuwapelekea zawadi ndogondogo.

 

 

Imeandaliwa na: Pd. Lukas Mgaya, Mkurugenzi wa Mashirika ya Kipapa-Jimbo

 

Read more

KONGAMANO LA UTOTO MTAKATIFU 26 – 29 DESEMBA 2024, MPANDA

Katika jimbo la Mpanda, kongamano lilianza tarehe 26 – 29 Desemba 2024. Tarehe 26 ilikuwa ni kwa ajili ya kuwasili. Tarehe 27 Des ilifanyika misa ya ufunguzi na bada ya hapo semina kwa watoto.

Watoto washiriki walikuwa 1,093, walezi 150, mapadre 12, masista 7 na Mha Baba Askofu na kufanyajumla kuu 1,263, ni sawa na ongezeko la asilimia 83 ya lengo kusudiwa.

Kwenye kongamano hilo, mada zilizotolewa ni mbili, ambazo ni;

  1. Unyanyasaji wa watoto – Pd Nicodemus Kyumana – Mkurugenzi wa PMS jimbo.
  2. Mazingira – Sr Mary Magdalene SND

 

Kilele cha kongamano kilikuwa tarehe 28 Desemba siku ya watoto mashahidi ambapo misa takatifu iliadhimishwa na Mha. Baba Askofu Eusebius Nzigilwa na kufuatiwa na chakuàla na burudani mbalimbali.

Tarehe 29 Desemba watoto walikuwa ni sehemu muhimu katika maadhimisho ya uzinduzi wa jubilei kuu kwa maandamano na misa takatifu iliyoadhimishwana Baba Askofu Eusebius Nzigilwa.

Baada ya Misa na chakula, na siku iliyofuata watoto walirudi maparokiani.

MAFANIKIO

  1. Ongezeko kubwa la ushiriki kwa watoto, walezi, mapadre na watawa.
  2. Ongezeko la ufahamu kwa watoto kutokana na mada wasilishwa.
  3. Ongezeko la hamasa la uundwaji wa kwaya za watoto.
  4. Ongezeko la ushiriki wa watoto wenye sare kwenye kongamano.

Tunamshukuru Mungu kwa ufanisi wa kongamano hili na tunatazamia maboresho na ufanisi mkubwa kwenye kongamano lijalo.

 

 

 

 

Imeandaliwa na: Pd. Nicodemus Kyumana, Mkurugenzi wa Mashirika ya Kipapa- Jimbo

Read more

TAARIFA YA KONGAMANO LA WATOTO JIMBO KATOLIKI LA MAFINGA

Tunamshukuru Mungu  kwa   zawadi  ya  uhai,  neema   na baraka  nyingi   atujaliazo  kila   siku  hadi tumehitimisha Kongamano  letu. Tunamshukuru pia kwa zawadi ya miaka 2025 ya Kuzaliwa Mwokozi wetu Yesu Kristo   ambaye ni zawadi ya Matumain i kwetu sisi wanadamu.

Washiriki

Kongamano letu limefanyika kwa siku   Tano na walikusanyika  watoto 902 na  walezi wao 74 kutoka Parokia zote za Jimbo Katoliki la Mafinga

Mada na Wakufunzi

Mada zilizowasilishwa ni kama ifuatavyo:  Wito –  Sr. Kil iana Sanga (CST), Mashirika ya Kipapa -Sr. Anagladness Mrumah (C.O.L.U, Fadhila – Pd. Gosbert Mlambia, Ulinzi na Usalama wa Watoto – Pd. Martin Mhavile, Yubilei Kuu 2025 – Pd. Paulo Wissa.

Mafanikio

Watoto walifanikiwa kupata mafundisho  juu   ya   Mashirika ya Kipapa,   Wito,  Fadhila Ulinzi na Usalama wa Mtoto na Dhamira ya Ybilei Kuu 2025. Pia watoto wamepata Sakramenti ya Kitubio na kuhimizwa juu ya majiundo kiroho na Kimaadili. Vilevile watoto walikula, walicheza, kuimba  na  kusali  pamoja  kwa  furaha.  Tukiongozwa  na  Baba  Askofu  wetu,  Vincent Cosmas Mwagala, tuliadhimisha 03/01/2025 Sherehe ya Watoto Mashahidi ikiwa ni Kilele cha Kongamano na Adhimisho la Yubilei Kuu 2025 Kijimbo  katika kundi la Watoto. Hakika tuliona uwepo wa Utukufu na Upendo wa Mungu kati ya watoto katika furaha yao ya kukusanyika Pamoja ndani ya Uzuri wa Mtoto Yesu. Furaha na Shangwe zilitanda Siku zote tano za Kongamano letu.

 

 

 

Imeandaliwa na: Pd. Gosbert Mlambia, Mkurugenzi wa Mashirika ya Kipapa- Jimbo

Read more